Magazeti leo Septemba 15,2026

Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imewapa siku 30 wataalamu wenye malimbikizo ya ada kukamilisha malipo yao, ikionya kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo watafutiwa usajili bila taarifa nyingine.








Akizungumza na waandishi wa habari Septemba 14, 2026 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB, CPSP. Godfred Mbanyi, amesema,hatua hiyo inalenga kuwawezesha wataalamu kukamilisha ada zao kabla ya Bodi kuanza ukaguzi katika ofisi za umma na binafsi mikoani baada ya kumalizika kwa siku hizo 30.

Amebainisha kuwa,mtaalamu yeyote anayefanya kazi za Ununuzi na Ugavi bila kusajiliwa na Bodi anavunja sheria, akisisitiza kuwa usajili huo unahusu sekta ya umma na binafsi.

Amesema, kila mtaalamu aliyesajiliwa anawajibika kulipa ada kwa mujibu wa sheria na kanuni za PSPTB, huku mtaalamu anayeshindwa kulipa ada kwa kipindi cha miezi 24 akitakiwa kufutiwa usajili na jina lake kuondolewa kwenye daftari la Bodi.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here