NAIBU Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma tayari amewasili nchini Vietnam kushiriki Fainali ya Mlimbwende wa Dunia (Miss World 2026).
Katika fainali hizo zitakazofanyika leo Septemba 5,2026, Naibu Waziri Mwinjuma atapokea bendera ya mashindano hayo kuashiria uwenyeji wa Tanzania kwa mwaka 2027.Katika fainali ya leo, Tanzania inawakilishwa na Mlimbwende Latricia Ian Sawe.





