Azam FC yaingia mkataba wa miaka mitatu na Omar Abdikarim Nasser kuwa Kocha Msaidizi mpya

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

UONGOZI wa Azam FC umeingia mkataba wa miaka mitatu na Omar Abdikarim Nasser kuwa Kocha Msaidizi mpya.

Ujio wa Nasser aliyesaini mkataba mbele ya Ofisa Mtendaji Mkuu, Abdulkarim Amin 'Popat', ni sehemu ya mapendekezo ya Kocha Mkuu, Abdihamid Moallin.
Nasser amewahi kufanya kazi katika nchi mbalimbali, mara ya mwisho 2019, akiitumikia moja ya vigogo vya nchini Qatar, Al Sadd, akiwa kama mchambuzi wa mechi (analyst) kabla ya kufanya majukumu kama hayo akiwa Al Duhail ya huko pia.

Al Sadd ni moja ya timu kubwa nchini humo, iliyokuwa ikinolewa na gwiji wa zamani wa Hispania, Xavi Hernandez, kabla kurejea Barcelona, akiwa kama Kocha Mkuu.
Mbali na kufanya kufanya kazi nje ya Taifa lake Somalia, pia alikuwa Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa ya Somalia kuanzia mwaka jana hadi sasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news