Mfanyakazi wa kulisha ng'ombe amuua mfanyakazi wa ndani

NA DIRAMAKINI

KIJANA ambaye alikuwa mfanyakazi wa kulisha ng'ombe amemuua msichana wa kazi za ndani kwenye nyumba waliyokuwa wakifanya kazi pamoja huku chanzo kikiwa bado hakijafahamika.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, ACP Pius Lutumo amesema kuwa, mtuhumiwa na marehemu walikuwa wakifanya kazi kwa mtu aliyefahamika kwa jina moja la Samwel.

Amesema kuwa, mtuhumiwa ambaye jina limehifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi umri wa miaka 27 alimuua Dawiya Mshihiri (30) kwa kumshambulia na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili.

"Mtuhumiwa baada ya tukio hilo alijaribu kujiua kwa kunywa sumu, lakini hakufanikiwa na kukamatwa na kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi kwa matibabu akiwa chini ya ulinzi wa polisi,"amesema Lutumo.

Aidha, amesema kuwa mtuhumiwa na marehemu walikuwa wakifanya kazi kwenye nyumba moja na Polisi wanaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.

Amebainisha kuwa, mara upelelezi utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria na anawasihi wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news