Mahakama ya Mwanzo Nyakibimbili yakamilika

NA AHMED MBILINYI

UJENZI wa Mahakama ya Mwanzo Nyakibimbili wilayani Bukoba, Mkoa wa Kagera umekamilika na tayari Mkandarasi kutoka Kampuni ya RK Solutions LTD, Mhadisi Gabriel Kami ameshakabidhi jengo jipya la Mahakama hiyo.
Hafla ya makabidhiano ya jengo hilo yalifanyika hivi karibuni baada ya timu ya washauri elekezi wa mradi kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wakiongozwa na Mhandisi Msanifu Majengo, Jafari Salehe na Timu ya Wahandisi kutoka Kitengo cha Ujenzi Makao Makuu ya Mahakama kufanya ukaguzi.

Viongozi kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Bukoba pamoja na viongozi wa eneo husika walikuwepo kushuhudia ukaguzi na makabidhiano hayo.
Mkandarasi kutoka Kampuni ya RK Solutions LTD, Mhadisi Gabriel Kami akimkabidhi funguo Kaimu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Mhe. Andrew Kabuka kama ishara ya makabidhiano ya jengo la Mahakama ya Mwanzo Nyakibimbili mara baada ya ujenzi wake kukamilika.

Kukamilika kwa ujenzi huo ni utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Mahakama 2020/2021 – 2024/2025 katika uboreshaji wa huduma zake kwa wananchi, ikiwemo kuimarisha miundombimu ya majengo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa makabidhiano hayo, Mhadisi Kami na Mhadisi Salehe wamesema jengo hilo limekamilika kwa asilimia 100, hivyo kushauri viongozi wa Mahakama kuanza kulitumia.
Picha ya pamoja kati ya Mkandarasi kutoka Kampuni ya RK Solutions, timu ya washauri elekezi wa mradi kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), timu ya Wahandisi kutoka Kitengo cha Ujenzi Makao Makuu ya Mahakama, viongozi kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba pamoja na viongozi wa eneo husika.

Akipokea jengo hilo kwa niaba ya Mtendaji wa Mahakama Kanda Bukoba, Bw. Lothan Simkoko, Kaimu Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, Mhe. Andrew Kabuka amewashukuru wataalamu hao kwa kukamilisha ujenzi huo. Ameahidi Mahakama itaanza kulitumia jengo hilo hivi karibuni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news