DCEA yakamata kilo 767.2 za dawa za kulevya, watuhumiwa 21 Dar, Pwani na Tanga

NA GODFREY NNKO

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imekamata zaidi ya kilo 767.2 za dawa za kulevya aina mbalimbali wakiwemo watuhumiwa 21.
Hayo yamesemwa leo Aprili 22,2024 na Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Amesema, dawa hizo zilikamtwa kwa nyakati tofauti kupitia operesheni iliyofanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga kuanzia Aprili 4 hadi 18, mwaka huu.

Kamishna Jenerali Lyimo amesema, kati ya dawa hizo zilizokamatwa Heroine ni kilogramu 233.2, Methamphemine kilogramu 525.67 na Skanka kilogramu 8.33.

"Watuhumiwa 21 wamekamatwa kuhusika na dawa hizo za kulevya, baadhi yao wamefikishwa mahakamani na wengine watafikishwa taratibu za kisheria zitakapokamilika,"amefafanua Kamishna Jenerali Lyimo.

Amesema, watuhumiwa wanaowakamata wengi wapo katika kundi la vijana kuanzia miaka 20 hadi 35.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news