Watakiwa kumiliki ardhi kisheria

SINGIDA-Wananchi wa Kata ya Unyamikumbi, Singida wamehimizwa kuhakikisha wanamiliki ardhi kisheria na kuweka alama za kudumu za mipaka ili kuepusha migogoro ya ardhi.
Akitoa elimu hiyo, Mkaguzi wa Polisi Kata ya Unyamikumbi, Inspekta Saidi January amesisitiza matumizi ya njia sahihi za usuluhishi pale migogoro inapotokea na umuhimu wa kuhudhuria elimu ya sheria mara kwa mara.

Pia,amekemea vikali tabia ya kuuza eneo moja kwa watu zaidi ya mmoja, akieleza kuwa ni kinyume cha sheria na chanzo cha migogoro katika jamii.
Wananchi wamekumbushwa kutoa taarifa za uhalifu kwa wakati ili kulinda amani ya maeneo yao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here