Kamati ya Bunge yaridhishwa na ujenzi ofisi ya TAKUKURU Nyang’hwale, yawapongeza viongozi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na TAKUKURU

NA VERONICA MWAFISI

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria imewapongeza Viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watendaji wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2025 kuhusiana na mapambano dhidi ya rushwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati hiyo mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita.

Kamati ya Bunge yawapongeza viongozi wa Ofisi ya Rais-UTUMISHI na TAKUKURU kwa utekelezaji mzuri wa ilani, yaridhishwa na ujenzi Ofisi ya TAKUKURU Nyang’hwale.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 14 Machi, 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakati wa ziara ya Kamati hiyo iliyolenga kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mara baada ya Kamati hiyo kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’wale, Mkoani Geita.

Akizungumza kwa niaba ya Kamati yake, Mhe. Dkt. Ndumbaro amesema CCM ilipokuwa inaomba kura kwa wananchi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 iliahidi mambo mengi ikiwemo kupambana na rushwa na kuitokomeza, jambo ambalo limetekelezwa kwa ufasaha kwa kujenga Ofisi za TAKUKURU katika maeneo mbalimbali nchini na kuanzisha klabu za wapinga rushwa mashuleni.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa klabu ya wapinga Rushwa Wilaya ya Nyang’wale, Mkoani Geita.

Serikali ya Awamu ya Sita inatekeleza Ilani, tumeona Ilani imetekelezwa kweli kweli katika kuzuia na kupamba na rushwa. Chama kiliahidi, sisi kama Wabunge jukumu letu ni kukagua kuona imetekelezwaje, hapa tunaona ilani imetekelezwa kwa asilimia 100, kwani tumeridhishwa na ujenzi huu wa Ofisi ya TAKUKURU Nyang’hwale,” ameongeza.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (kulia) akifuatilia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakipata maelezo ya Mradi wa ujenzi wa jengo lililojengwa katika Wilaya ya Nyang’hwale, mkoani Geita mara baada Wajumbe wa Kamati hiyo kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU. Watatu kutoka kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.

Mhe. Dkt. Ndumbaro ametoa maelekezo kwa Viongozi wa Ofisi hiyo kuendelea kusimamia ubora wa majengo yote yatakayojengwa na ujenzi wa ofisi zote za TAKUKURU nchini.

Akitoa maelezo ya awali ya utekelezaji wa mradi wa jengo la TAKUKURU Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameishukuru Kamati hiyo kwa maelekezo na miongozi mbalimbali ambayo wamekuwa wakiyatoa na kufanikisha utekelezaji mzuri wa majukumu ya Ofisi anayoiongoza ikiwemo ujenzi wa jengo hilo la TAKUKURU.

Mhe. Kikwete amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 386 ambapo utekelezaji wake ulifuata taratibu zote za manunuzi kwa kuongozwa na sheria ya manunuzi na umetekelezwa kupitia Force Account.

Mhe. Kikwete ameahidi kuendelea kutekeleza maelekezo yote ambayo yatatolewa na Kamati hiyo ili kuboresha utendaji kazi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa maendeleo ya taifa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Katikati) akifuatilia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila.
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila akieleze utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria mara baada ya Wajumbe hao kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo lililopo Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Wakuu wa Vitengo wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU lililopo Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Muonekano wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita ambalo Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria walitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo hilo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (wa pili kutoka kushoto) akifurahia jambo wakati walipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU, Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale, Mhe. Grace Kingalame.
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete (hayupo pichani) alipokuwa akitoa maelezo ya awali kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo kuzungumza na Watumishi wa TAKUKURU na Wananchi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Maafisa wa vyombo vya Ulinzi na Usalama wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoani Geita.
Sehemu ya Watumishi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wakimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao mara baada ya Kamati yake kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU lililopo Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuingia katika ofisi za TAKUKURU ambayo ni moja ya Taasisi zilizopo chini ya ofisi yake ambapo Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria ilitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa jengo la TAKUKURU Wilaya ya Nyang’hwale mkoani Geita.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa TAKUKURU, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Chalamila amesema tangu kuanzishwa kwake TAKUKURU imekuwa ikikabiliwa na uhaba wa majengo lakini katika kutatua changamoto hiyo, Serikali imekuwa ikijitahidi kujenga na kutafuta majengo ya kupanga ili kutekeleza majukumu yake ya kuzuia na kupamba na rushwa.

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuweka kipeumbele na kuchukua hatua mbalimbali ili kuiimarisha taasisi hiyo katika utekelezaji wa majukumu yake ikiwemo kutenga bajeti kwa ajili ya kujenga majengo yenye miundombinu ya kisasa na kukarabati majengo ya zamani,” ameongeza Bw. Chalamila.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here