Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, amekutana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Biashara wa Jimbo la Shandong, Mheshimiwa Wang Lei, ambapo wamejadili masuala mbalimbali ya kimkakati pamoja na namna ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi.
Katika mazungumzo yao, viongozi hao walijikita katika kuhamasisha uwekezaji kati ya Tanzania na Jimbo la Shandong nchini China, hususan katika sekta muhimu za maendeleo. Prof. Mkumbo ameridhia mapendekezo na makubaliano yaliyowasilishwa, ikiwa ni pamoja na kuanzisha na kuimarisha ushirikiano katika sekta za kimkakati kama vile viwanda, madini, kilimo na utalii.
Aidha, mbali na kikao hicho, Prof. Kitila alifanya mazungumzo ya kina na wawekezaji mbalimbali wanaotarajia kuwekeza nchini Tanzania.
Miongoni mwao ni wawekezaji wakubwa katika sekta ya saruji kutoka Kampuni ya Anhui Conch Cement Co., Ltd, wakiongozwa na Bw. Terry Chu, ambao wamevutiwa kuwekeza Tanzania na ndio nchi ya kwanza kwao katika nchi za Afrika.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


















