DODOMA-Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mheshimiwa Hamza S. Johari ameungana na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi katika kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi.
Hafla hiyo imefanyika katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, leo Machi 27, 2026.Aidha,misa ya kuaga mwili imeongozwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mwigulu Lameck, ambapo viongozi mbalimbali wa kitaifa walihudhuria kutoa heshima zao za mwisho.
Mheshimiwa Lukuvi alifariki dunia Machi 25,2026 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma alipokuwa akipatiwa matibabu.
Tags
Habari
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Ratiba ya Mazishi ya Lukuvi
William Vangimembe Lukuvi



