DAR-Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), kwaniaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Kampuni ya PLASCO inayojihusisha na uzalishaji wa mabomba ya plastiki yanayotumika katika miundombinu ya maji na gesi, ukiongozwa na Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo, Bw. Dario Manlubatan, akiambatana na Meneja wake wa Masoko, Bi. Edith James, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam, ambapo walijadili mchango wa sekta ya viwanda katika kukuza uchumi wa nchi.
Mhe. Luswetula aliahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi, kushughulikia changamoto zao, pamoja na kuendelea kuweka mazingira rafiki ya ufanyaji biashara na uwekezaji ili kukuza maendeleo ya uchumi wa nchi.
Kwa upande wa Kampuni ya Plasco, Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo, Bw. Dario Manlubatan, alieleza utayari wao wa kushirikiana na Serikali katika miradi ya kimkakati, ikiwa ni pamoja na kuleta ubunifu na utaalamu utakaosaidia kuimarisha miundombinu ya miradi ya maji na kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa jamii.



