Magazeti leo Aprili 1,2026

Wizara ya Maji kwa kushirikiana na taasisi binafsi imeandaa mafunzo kuhusu usalama wa mabwawa Ili kuhakikisha mabwawa yanaendelea kuwa salama kwa matumizi yaliyokusudiwa hapa nchini.
Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji, Wizara ya Maji Bw. Robet Sunday akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji katika mkutano na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano Wizara ya Maji Mtumba jijini Dodoma ametaja taasisi zinazoshirikiana na Wizara ya Maji kuwa ni Chemba ya Migodi Tanzania (CMT) na Kampuni ya Uhandisi ya City.

Mafunzo hayo yanatarajia kufanyika jijini Mwanza kuanzia Oktoba 21 hadi 23, 2026 yakilenga kuendelea kutoa elimu kwa wadau na wataalamu wa mabwawa ili kuhakikisha usanifu, ujenzi na uendelezaji wa mabwawa ya maji na mabwawa ya tope sumu yana viwango ili kulinda mazingira na vyanzo vya maji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here