Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amewataka wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu nchini na vijana kuendelea kulinda na kutetea misingi ya Muungano iliyoachwa na Waasisi.

Mhe. Mhandisi Masauni ameyasema hayo Aprili 06, 2026 jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongamano maalum la kumuenzi aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.
Waziri Masauni amesema mwasisi huyo wa Muungano ameacha alama na historia ya kudumu kwa vizazi vya sasa na vijavyo, juhudi zilizotokana na mchango alioutoa katika kuwaunganisha Watanzania na kupambania maslahi ya wananchi wanyonge.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo
























