VIDEO:Mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Tanzania Olympic Committee (TOC), Rahim Kalyango aibua mapya mchakato wa uchaguzi

DAR-Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Tanzania Olympic Committee (TOC), Rahim Kalyango, amelalamikia kuvunjwa kwa kanuni za uchaguzi pamoja na kukiukwa kwa baadhi ya vifungu vya kisheria vinavyoongoza mchakato wa uchaguzi wa kamati hiyo.
Akizungumza katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Kalyango alisema kuwa kuna taratibu muhimu ambazo hazikufuatwa ipasavyo katika maandalizi ya uchaguzi huo, na hivyo kuhatarisha uhalali na uwazi wa mchakato mzima.

Kutokana na hilo, ameomba serikali kuingilia kati na kuchukua hatua stahiki ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa kuzingatia sheria, misingi ya haki, na usawa kwa wagombea wote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here