Magazeti leo Mei 24,2026

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Edith Swebe amewaongoza Maafisa, Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali katika hafla ya kumuaga aliyekuwa Sajenti wa Jeshi la Polisi Faustina Kunjumu, ambaye amemaliza muda wake wa utumishi ndani ya Jeshi la Polisi.
Hafla hiyo imefanyika kwa lengo la kutambua na kuthamini mchango wa Sajenti Kunjumu katika kulijengea Jeshi la Polisi heshima na kuimarisha utoaji wa huduma kwa wananchi wakati wa kipindi chake chote cha utumishi.
Kamanda Swebe amepongeza nidhamu, uadilifu na kujituma kwa Sajenti Kunjumu, akisema kuwa maadili aliyoonyesha yanapaswa kuwa mfano kwa askari wengine waliopo kazini na wanaoendelea na majukumu yao katika kulinda usalama wa raia na mali zao.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here