Klabu ya Young Africans SC (Yanga) sasa ipo huru kufanya usajili wa wachezaji wapya kwa ajili ya mashindano mbalimbali ya ndani na kimataifa, ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya uongozi wa klabu hiyo kuthibitisha kuwa hakuna deni lolote linaloizuia kusajili.
Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rogers Gumbo, amesema changamoto iliyosababisha klabu kuonekana kwenye orodha ya FIFA ya vilabu vilivyofungiwa usajili ilitokana na kutokamilika kwa baadhi ya taarifa na nyaraka zilizokuwa zinahitajika na FIFA pamoja na CAF, na si deni la kifedha kama ilivyodhaniwa na wengi.
Kwa mujibu wa Gumbo, Mei 31, 2026 ilikuwa siku ya mwisho ya muda wa ziada uliotolewa kwa klabu zilizokuwa na mashauri ya malipo, ambapo Yanga imefanikiwa kutimiza matakwa yote yaliyokuwa yanahitajika.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo


















