NA DIRAMAKINI
LEO Agosti 7,2026 Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazindua rasmi kielelezo cha faida rejea ya dhamana za serikali (Tanzania Sovereign Yield Curve) katika Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.
"Hii ni hatua muhimu katika kuendeleza soko la ndani la dhamana za Serikali, ikitarajiwa kuleta uwazi sokoni, kuboresha upatikanaji wa bei halisi za soko, kuchochea ukuaji wa soko la upili na kuweka msingi thabiti na wa kuaminika katika kupanga bei za dhamana za Serikali pamoja na bidhaa nyingine za kifedha."