Wazazi tushirikiane kudhibiti utoro shuleni

PWANI-Mkaguzi wa Polisi Anna Mawala, Msimamizi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani, Agosti 15, 2026 amewataka wazazi kudhibiti utoro wa wanafunzi shuleni.
Hayo yamesemwa katika kikao cha wazazi na uongozi katika shule ya Sekondari Msangani Government pamoja na Polisi Kata, ambapo Mkaguzi Mawala amewataka wazazi kufatilia nyendo za watoto wao na makundi wanayojumuika nayo ili kujua ni ya aina gani.

"Wazazi wengi wamekuwa wavivu kufatilia maendeleo ya watoto wao na kuwaachia jukumu waalimu peke yao, kitendo ambacho kinawapa mwanya wanafunzi kujiunga na makundi mabaya yanayopelekea mmonyoka wa maadili kwakukosa Usimamizi sahihi toka nyumbani, wazazi wengi wamekuwa na madai ya utafutaji wa kipato kwa muda mwingi zaidi na kushindwa kuwafatilia watoto wao,"amesema Mawala.

Kupitia kikao hicho kilichojumuisha wazazi, walezi, uongozi wa shule pamoja na Polisi Kata wameeazimia kuungana kwa pamoja ili kutokomeza utoro mashuleni ndani ya Kata ya Msanagani na kuboresha taaluma na kupandisha ufaulu kwa kuwafatilia wanafunzi wote kuanzia nyumbani, mtaani na shuleni.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here